Wednesday, October 26, 2011

WATU ZAIDI YA 35 WANUSURIKA KUFA BAADA YA BASI LA DELUX WALILOKUWA WAKISAFIRIA KUPINDUKA NA KUUNGUA ENEO LA KONGOWE!

Watu
zaidi ya 35 wamejeruhiwa katika ajali yak basi iliyotokea maeneo ya
Kongowe mkoani Pwani. Mashuhuda wamelitaja basi hilo kuwa ni DELUX
coach, ambalo lililokuwa linatoka Dar es salaam, kuelekea mkoani Dodoma,
mchana wa jana , ambapo lilipinduka na kuungua huku ndani likiwa na abiria
na hivyo kuzusha hofu kwa ndugu na jamaa ambao wamesafirisha jamaa zao
katika gari hilo.

Afisa habari hospitali ya
Tumbi mkoani Pwani, Bi rose Mtei anaweka wazi idadi hiyo ya majeruhi
waliopokelewa hospitalini hapo na hali za majeruhi.

Hata hivyo ofisa uhusiano
huyo, alikiri kutopokelewa kwa maiti yoyote katika hospitali hiyo, na
jitihada za kutafuta kamanda wa polisi mkoa ili kuzungumzia hilo
hazikufanikiwa baada yak simu yake kuita bila mafanikio.

No comments: