Jeshi la Majini la Tanzania lafanyakazi na majirani kupiga vita uharamia
Omar alisema
sheria za kimataifa zinauelezea uharamia chini ya mapatano mawili makuu –
Kifungu nambari 15 cha Mapatano ya Bahari Kuu ya mwaka 1958 na Kifungu
cha 101 cha Mapatano ya Umoja wa Mataifa wa Sheria za Bahari ya mwaka
1982. Vifungu hivi vinauelezea uharamia kuwa tendo la vurugu, ukamataji
wa nguvu na hasara zinazofanya kwa madhumuni ya siri na mabaharia au
abiria wa meli binafsi katika bahari kuu dhidi ya meli nyingine.
Katika mahojiano ya pekee kwa mtandao wa habari wa Sabahi huko Dar es
Salaam hapo Jumatatu (tarehe 9 Januari), kamanda alisema kuwa juhudi za
vita dhidi ya uharamia vimepunguza matukio ya uharamia katika maeneo ya
bahari ya Tanzania kutoka matukio 30 mwaka 2006 hadi tisa mwaka 2011.
Sabahi: Vipi unaweza kuelezea jukumu la jeshi lako la majini katika kupambana na maharamia wa Somali?
Maj. Gen. Said Shaaban Omar: Uharamia
umekuwepo
ulimwenguni kote kwa miaka mingi; kitendo cha kwanza cha uharamia
kiliripotiwa katika karne ya 13. Karibu na hapa petu, uharamia
ulichomoza sura yake mbaya miaka michache baada ya kuanguka kwa serikali
ya Generali Siad Barre huko Somalia. Tukio hili kwa bahati mbaya
mwishowe limepelekea kutokuwepo kwa uongozi.
Hata hivyo, tatizo lilizidishwa na meli za kigeni zilizokuwa
zikiwanyanyasa wavuvi wa Kisomali katika maeneo ya bahari yao. Na kama
sehemu ya jawabu yao, wavuvi wa Kisomali mara moja moja walianza
kuzishambulia meli za uvuvi za kigeni na kudai kulipwa fedha. Mwisho
waliona kuwa raha biashara yao hii na mengine yote ni historia, kwa vile
uharamia sasa umeondoka katika maeneo ya baharí ya Somalia – na
kukaribia India kwa kaskazini na Msumbiji kwa kusini.
Sasa turudi kwenye suala letu. Tatizo la uharamia katika maeneo ya
baharí yetu lilianza mwaka 2006, na kuanzia hapo, kitengo chetu cha
jeshi la baharini limeishakamata jumla ya maharamia wa Kisomali 25.
Tumeieshawakabidhi polisi ili kuchukulia hatua zifaazao ili sheria
ichukue mkondo wake.
Mnamo mwaka 2006, tulikuwa na matukio 30 ya uharamia katika maeneo ya
bahari yetu ambayo kitengo changu cha jeshi la baharini
limeyashughulikia. Habari nzuri ni kuwa matukio yote hayo 30, kitengo
kilimudu kulishughulikia tatizo hili kabla hayajatushinda, katika hatua
ya maharamia kufikia kuomba fedha kutoka meli walizokuwa wanazishikia
visivyo halali kiliweza kuyadhibiti. Bila shaka, matukio hayo 30 ni
pamoja na ukamataji na habari tulizopokea katika kitengo chetu cha jeshi
la baharini na meli zilizowagundua maharamia hao.
Habari nzuri ni kuwa tangu kuanza kwa kampeni mwaka 2006, matukio ya
uharamia yamepungua kutoka 30 hadi tisa mwaka 2011. Kupungua kwa matukio
haya ya uharamia katika maeneo ya baharí yetu ni matokeo ya juhudi zetu
za kupambana nayo bila huruma.
Lakini hii si kusema kuwa imekuwa rahisi; kinyume chake. Tumekuwa
tukishughulikia changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na mambo mengine,
maharamia wamekuwa wakitumia mbinu kutoka mashambulizi hadi kupanda meli
kwa kujificha usiku. Kitu kama hicho kinaweza kusemwa kuhusu matumizi
yao ya silaha, kutoka bunduki aina ya AK-47 hadi mashini gani na silaha
nyingine nzito. Imetubidi tuende nao sambamba; vinginevyo, ingekuwa
tumepoteza vita hii.
Changamoto nyingine ni, bila shaka, linawasilishwa na ukanda wa
mwambao, ambao una kilomita 1,440. Hii ni changamoto kubwa kwa watu na
vifaa. Si rahisi kulinda eneo kubwa kama hilo.
Sabahi: Ni changamoto gani za kiuchumi katika kupambana na maharamia?
Omar: Tangu kuanza kwa vitendo vya uharamia katika eneo la
bahari yetu, kumekuwepo na kiwango kikubwa cha upungufu wa meli kubwa
katika bandari za Tanzania, hasa Dar es Salaam. Meli zimezidi kuchukua
tahadhari kabla ya kusafiri kuja Tanzania kutokana na kuongezeka kwa
vitendo vya uharamia katika maeneo ya bahari zetu. Meli zenye hatua za
usalama wa kutosha pekee zinaendeshwa kwenda Tanzania, kumaanisha
upunguaji wa uingizaji nchini. Uwekaji wa hatua za ziada za usalama
kwenye meli ulisababisha gharama za ziada za uendeshaji kwa meli hizo --
na mwishoni wanaoingiza bidhaa nchini wanalipa hizo gharama.
Kwa ufupi, hili limepelekea kuongezeka kwa bei za bidhaa tunazoagiza.
Mfano mzuri ni kuongezeka kwa bei ya gesi ya majimbani miezi mitatu
iliyopita, kulikosababishwa na kushuka sana kwa meli zinazobeba gesi
zinazokuja bandari ya Dar es Salaam. Hali hii ilisababishwa na
shambulizi lililoshindwa lililofanywa na maharamia wa Somalia kwa meli
iliyokuwa imebeba gesi kufikia Dar es Salaam. Tukio hili lilitokea
katika maeneo ya bahari ya Tanzania. Kwa bahati nzuri, tulilizima tukio
hili mapema.
Sabahi: Ni maeneo gani mengine yameathiriwa na uharamia?
Omar: Sehemu ya sekta ya utalii vile vile imeathiriwa na
tatizo la uharamia. Hakuna chochote kinachoelezea kitu hiki kama meli za
kifahari za kitalii, meli za kifahari za abiria zinazopeleka watalii
kuzunguka ulimwengu. Mwaka 2006 pekee, kulikuwa na meli za aina hiyo 26
zilizozuru Tanzania. Hata hivyo, idadi hii imeshuka na kufikia meli
mbili mwaka 2010 na hakukuwa na meli hata moja mwaka 2011. Yote haya
yanaweza kuwa yamechangiwa na vitendo vya uharamia.
Maeneo mengine ni pamoja na uwekezaji wa kigeni wanaotafuta gesi na
mafuta katika maeneo ya baharí ya Tanzania. Mpaka sasa, kumekuwepo na
majaribio ya uharamia kwa meli zinazoendesha utafutaji wa gesi na mafuta
sehemu ya kusini ya mwambao wa nchi, karibu na Visiwa vya Mafia. Hata
hivyo, katika mara zote mbili, meli zetu za jeshi la majini ziliweza
kuwafukuza maharamia, lakini vile vile zilifanya ukamataji saba.
Sabahi: Kumekuwepo na taarifa kuhusu mazoezi ya pamoja ya
kijeshi yanayoendeshwa na Jeshi la Ulinzi la Tanzania (TPDF) na Kikosi
cha Ulinzi cha Kenya. Mazoezi haya yamekuwa aina ya ushirikiano katika
bahari?
Omar: Tumekuwa na mashirikiano ya karibu na wenzetu wa
Kenya katika maeneo yote yanayohusiana na vita dhidi ya uharamia katika
maeneo ya bahari yetu. Karibu kila siku tunawasiliana nao, kubadilishana
habari kuhusu kile kinachoendelea katika Bahari la Hindi. Daima
tulibadilishana habari kila mara kunapokuwepo na sababu za kuaminika
kuwa adui wetu wa pamoja amekimbilia upande wa pili, mbali na mipaka ya
kisheria. Kwa neno moja tu, maharamia hawana pa kujificha!
Mbali na Kenya, vile vile tumekuwa tukifanyakazi kwa karibu na
majeshi ya wenzetu wa eneo la SADC (Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za
Kusini mwa Afrika). Pamoja na kuwa na uhusiano wa kikazi wa karibu na
wajumbe wa nchi za SADC, TPDF vile vile ina mahusiano mazuri na wajumbe
wanne wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki – Uganda, Rwanda, Burundi na
Kenya. Jeshi la majini la Tanzania vile vile limekuwa likifanyakazi kwa
karibu na wenzao wa Msumbuji katika eneo la kusini.
No comments:
Post a Comment