Sunday, March 25, 2012

 Lundenga: Ni mwanzo wa mafanikio ya Redds Miss tz 2012 Imani MakongoroHUENDA mfumo huu ukawa mgeni lakini ukweli ni kwamba, Miss World kuanzia mwaka huu na kuendelea itakuwa ikifanyika Agosti na washiriki watatakiwa kuripoti kambini mwezi mmoja kabla yaani Julai.Utaratibu huu umetokana na mabadiliko ya kalenda ya waandaaji wa mashindano hayo, ambapo miaka iliyopita shindano hilo lilikuwa likifanyika Desemba na washiriki kutakiwa kuripoti Novemba.Kulingana na mabadiliko hayo Tanzania itatuma mwakilishi kwenye mashindano ya dunia ya mwaka huu, atapatikana kwa kuwapambanisha warembo 10 jukwaani wakati huo huo mchakato wa kumpata Redds Miss Tanzania 2012 utakuwa ukiendelea kama kawaida.    Miss Tanzania mbili ndani ya mwaka mmoja:Hashim 'Uncle' Lendenga  anasema kwamba, wameamua kufanya hivyo ili Tanzania iweze kuwa na mwakilishi kwenye Miss World  ya 2012."Miss Tanzania hufanyika  Septemba miaka yote, mabadiliko ya kalenda ya Miss World yanaonyesha shindano litakuwa likifanyika Agosti kila mwaka na washiriki kutakiwa kuwasili China (yanapofanyika mashindano) Julai," alisema.    Nani atapeperusha bendera ya Tanzania kwenye Miss World 2012."Tutafanya shindano dogo litakalohusisha warembo 10 kwenye fainali na mshindi ndiye atakuwa mwakilishi wetu kwenye Miss World," anasema Lundenga.Anasema mchakato wa kumpata mlimbwende huyu utakuwa wa usaili ambapo watawafanyia usaili warembo kati ya 40 hadi 50 ili kupata 10 bora watakaowekwa kambi ya siku chache kabla ya fainali itakayofanyika Mei.     Mchakato halali wa Miss Tz utakuwaje."Wakati hayo yakiendelea pia mchakato uliozoeleka wa kumpata Redds Miss Tz 2012 utakuwa ukiendelea," anasema.Anasema zoezi hilo halitakuwa na tofauti na Miss Tz zilizopita ambapo mchakato utaanzia ngazi za vitongoji, kanda na hatimaye taifa katika fainali itakayowakutanisha warembo kati ya 28 na 29."Fainali itafanyika Septemba kama ilivyoada lakini mshindi atakayepatikana atapeperusha bendera ya Tanzania kwenye Miss World ya 2013 itakayofanyika Agosti," anasema.    Mabadiliko ya Miss World yameiathiri vipi tz."Kwanza yamevuruga ule utaratibu wa kumpata mwakilishi wetu kwenye Miss World ingawa Kamati iliamua kutumia utaratibu wa kutuma mwakilishi hivyo haijatuathiri sana," anasema.Anasema pamoja na hilo mabadiliko hayo yamevunja utaratibu wa mshiriki kupewa mwaka mmoja kwa kutoa'second chance' kwa warembo waliopita ambao wanavigezo kujaribu tena bahati yao na wale ambao bado lakini wana vigezo kuitumia nafasi hiyo."Mwakilishi wetu mwaka huu atakuwa na muda mfupi mno wa maandalizi kabla ya kuondoka kwenda kwenye fainali sambamba na kuwa kambini kwa siku chache tofauti na ilivyozoeleka," anasema.        Tanzania itanufaika vipi na mabadiliko hayo kwenye Miss World ya 2013.  Lundenga anasema pamoja na mabadiliko hayo kuiathiri Tanzania mwaka huu lakini pia  yatakuwa na manufaa kwa Redds Miss Tanzania 2012 kwenye Miss World ya 2013."Kwanza kabisa mrembo wetu atakuwa na muda mwingi wa kufanya maandalizi yake kabla ya kushiriki Miss World," anasema.Anasema pia mrembo huyo atakuwa na nafasi ya kufanya kazi za kijamii pamoja na kujifunza mbinu mbalimbali za kimataifa ambazo zitamuweka kwenye nafasi nzuri katika Miss World ya 2013."Mabadiliko hayo si kwa Redds Miss Tanzania 2012 hata kwa warembo wengine watakaofuata watakuwa na nafasi ya kufanya vizuri kwa kuwa watakuwa na muda mrefu wa maandalizi yao," anasema.Kwa mara ya kwanza Tanzania ilifanya vizuri kwenye Miss World ya 2005 kwa Nancy Sumari kuingia hatua ya tano bora akiwa miongoni mwa washiriki kutoka nchi 120 na kuiwezesha nchi kupanda kwenye chati ya viwango vya ubora vya urembo vya dunia.

No comments: