Sunday, March 25, 2012

Davina: Wapenzi wangu wengi walikuwa wa maneno

 KARIBU tena mpenzi msomaji wa SIDE B. Leo tunamalizia kuperuzi maisha ya upande wa pili ya mwigizaji wa sinema za Bongo, Halima Yahya ‘Davina’. Ili kujua nini amemalizia fuatana nami.

VIPI KUHUSU MAUMIVU KATIKA MAPENZI?
Davina: Mwanaume akitambua unampenda sana lazima ipo siku atakuumiza tu. Kwa kweli nimeshaumizwa sana, ila kwa sasa nafasi hiyo haipo tena.
JE, ANAMKUMBUKA MPENZI WAKE WA KWANZA?
Davina: Kama nilivyokwambia mara ya kwanza kuwa nilianza kutoa uroda mara baada ya kumaliza kidato cha nne, ila wale ambao nilikuwa na mapenzi ya stori wapo wengi.
ETI ANA BIFU NA NISHA?
Davina: Hapana mimi sina bifu na Nisha, labda yeye kama anatangaza ana bifu na mimi, lakini sina muda huo.
SIDE B: Kuna tetesi zisizo rasmi kuwa Nisha ana uhusiano wa kimapenzi na mzazi mwenzako aliyesababisha ukalale mahabusu Segerea, hujasikia hilo?
DAVINA: Haitakuja kutokea kwa sababu yule mwanaume mimi ndiye niliyemuacha. We unaona shepu ya kuachwa hii, hebu nitazame vizuri kwanza, sina shida ya kumpa mtu promo kupitia jina langu.
MAJUNGU JE?
Davina: Hakuna kitu kinachoniuma kama majungu, hasa kwa sisi wanawake wa Bongo Movie. Kwa kweli tuna ushoga wa ‘Kichina’, ukiwa naye anakuwa rafiki, mkiachana tu anakwenda kukuweka hadharani baadaye ukija kusikia huamini masikio yako.
ANASEMAJE KUHUSU MASTAA WA KIKE KUTOA URODA ILI WAPEWE NAFASI YA KUIGIZA?
Davina: Siwezi kuongopa, ni kweli hilo suala lipo na mimi nilishawahi kukumbana nalo, si kwenye sanaa tu hata maofisini mambo hayo yapo, mashuleni pia hayaepukiki.
MSOSI UNAOUZIMIA
Davina: Sina chaguo kwenye kula, napenda vyakula vingi.
ANAPENDA MWANAUME WA AINA GANI?
Davina: Napenda mwanaume mwenye mvuto, anayejua kumuenzi mpenzi wake na awe mtundu ‘uwanjani’ kipindi cha mechi.
NJE YA UIGIZAJI ANAFANYA NINI?
Davina: Kwa sasa sina ninalolifanya nje ya kuigiza lakini nina mpango wa kumiliki kampuni yangu pamoja na taasisi ambayo itawasaidia kina mama kujikwamua kimaendeleo.
KITU GANI ANACHOKIKUMBUKA KILA WAKATI?
 Davina: Ni siku niliyopanda karandinga kwenda Segerea, najuta maana mapenzi ndiyo yaliyonifanya nikalale kule, nisingekuwa na uhusiano na yule mtu hadi kuzaa naye nisingepata matatizo yale.
“Asikwambie mtu jela isikie tu kwa mwenzako, lakini usiombe ikukute wewe, ni kubaya mno hakufai hata kuhadithiwa.”
SIDE B: Nashukuru sana kwa ushirikiano wako Davina, Mungu akupe afya njema.
Davina:  Ahsante.

No comments: