Sunday, March 25, 2012

FAMILIA YA KAJALA YAKATAA MCHANGO WA WEMA

 KUFUATIA kesi ya kughushi hati ya fedha inayomkabili mumewe, Faraji Augustine Chambo, staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja, 26, aliyeko Gereza la Segerea, Dar es Salaam akisubiri hukumu, baadhi ya ndugu zake wameibuka na kudai kuwa hawahitaji kuona mchango wa mwigizaji mwenzake, Wema Sepetu.
Kwa mujibu wa chanzo makini cha Risasi Jumamosi, tamko hilo limekuja baada ya baadhi ya wasanii kuanza kuchangishana fedha kwa ajili ya kumuwekea dhamana Kajala ili asiendelee kusota gerezani.

 

NI UNAFIKI?

“Wema ndiye alikuwa mara nyingi akifurahia ndugu yetu kuhukumiwa, hivi karibuni alikuwa akimsema vibaya hadi kufikia hatua ya kugombana naye, atuletee mchango? Utakuwa ni unafiki tu hata hatuhitaji,” alisema ndugu wa karibu wa familia ya Kajala.
HUKUMU
Hukumu ya kesi hiyo iliahirishwa juzi Alhamisi hadi Jumatatu ijayo Machi 26, mwaka huu.
TUJIKUMBUSHE
Leo Kajala ametimiza siku nane tangu alipotupwa katika Gereza la Segerea Machi 16, mwaka huu ambapo alishikiliwa na maofisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kwa madai kuwa aliuza nyumba ya mumewe Faraji iliyokuwa na mgogoro ambayo walikuwa wakiichunguza maeneo ya Mbezi Salasala, Dar.

 WEMA ANASEMAJE?
Risasi Jumamosi lilimsaka Wema kwa njia ya kilongalonga cha kiganjani ili kumfikishia habari hiyo na kusikia anasemaje, lakini juhudi hizo ziligonga mwamba kufuatia simu yake kutokuwa hewani kila ilipopigwa.

No comments: