FAMILIA YA KAJALA YAKATAA MCHANGO WA WEMA
KUFUATIA kesi ya kughushi hati ya fedha inayomkabili
mumewe, Faraji Augustine Chambo, staa wa filamu za Kibongo, Kajala
Masanja, 26, aliyeko Gereza la Segerea, Dar es Salaam akisubiri hukumu,
baadhi ya ndugu zake wameibuka na kudai kuwa hawahitaji kuona mchango wa
mwigizaji mwenzake, Wema Sepetu.
Kwa mujibu wa chanzo makini cha
Risasi Jumamosi, tamko hilo limekuja baada ya baadhi ya wasanii kuanza
kuchangishana fedha kwa ajili ya kumuwekea dhamana Kajala ili asiendelee
kusota gerezani.
NI UNAFIKI?
“Wema ndiye alikuwa mara nyingi
akifurahia ndugu yetu kuhukumiwa, hivi karibuni alikuwa akimsema vibaya
hadi kufikia hatua ya kugombana naye, atuletee mchango? Utakuwa ni
unafiki tu hata hatuhitaji,” alisema ndugu wa karibu wa familia ya
Kajala.
HUKUMU
Hukumu ya kesi hiyo iliahirishwa juzi Alhamisi hadi Jumatatu ijayo Machi 26, mwaka huu.
Hukumu ya kesi hiyo iliahirishwa juzi Alhamisi hadi Jumatatu ijayo Machi 26, mwaka huu.
TUJIKUMBUSHE
Leo Kajala ametimiza siku nane tangu alipotupwa katika Gereza la Segerea Machi 16, mwaka huu ambapo alishikiliwa na maofisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kwa madai kuwa aliuza nyumba ya mumewe Faraji iliyokuwa na mgogoro ambayo walikuwa wakiichunguza maeneo ya Mbezi Salasala, Dar.
Leo Kajala ametimiza siku nane tangu alipotupwa katika Gereza la Segerea Machi 16, mwaka huu ambapo alishikiliwa na maofisa wa Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (TAKUKURU) kwa madai kuwa aliuza nyumba ya mumewe Faraji iliyokuwa na mgogoro ambayo walikuwa wakiichunguza maeneo ya Mbezi Salasala, Dar.
No comments:
Post a Comment