Sunday, March 25, 2012

UWOYA adhalilika

 IKIWA ni siku chache tangu mumewe, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ alipoondoka Bongo, Irene Pancras Uwoya anadaiwa kudhalilika ukumbini baada ya kigauni kifupi alichotinga kushindwa kumsitiri hivyo ‘kufuli’ lake kuwa nje nje, aya zifuatazo zina undani kamili.

Tukio hilo la kusikitisha lilichukua nafasi ndani ya Ukumbi wa Business Park Kijitonyama, Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo kulikuwa na ‘bethidei’ ya mwaka mmoja ya Klabu ya Bongo Movie.

MAPEDESHEE WAJIPITISHA
‘Shushushu’ wa gazeti hili aliwashuhudia wanaume hasa mapedeshee wakijipitisha mbele ya meza aliyokuwa amekaa Uwoya na mwigizaji mwenzake, Blandina Chagula ‘Johari’.
Hata hivyo, ilielezwa kuwa kilichomponza Uwoya ni kigauni alichovaa kifupi kilichosababisha nguo hiyo ya ndani nyeupe kuonekana kirahisi alipokuwa amekaa.
NENO LA WADAU
“Duh! Mama Krish (Uwoya) katoka bomba lakini kile kigauni kinamdhalilisha, kinaonesha kufuli yake nyeupe.
Ukweli ni kwamba angekuwepo Ndiku (mumewe) asingefanya hivyo kwa sababu angemlindia heshima,” alisema mmoja wa wadau waliomshuhudia staa huyo ambaye muda mwingi alikuwa kimya ukumbini humo.
UWOYA VIPI?
Jitihada za kuzungumza na Uwoya juu ya tukio hilo hazikuzaa matunda kufuatia simu yake kuita bila kupokelewa.
Hivi karibuni Ndiku alitimka Bongo na kwenda kwao Rwanda kujiunga na timu ya Rayon Sports huku akimwacha mkewe huyo na mwanaye Krish. 

No comments: