Sunday, March 25, 2012

Mchungaji anaswa akimuogesha mke wa mtu

AMA KWELI dunia imekwisha, makanisa, watumishi wa Bwana wanazidi kumtia hasira Mungu kila kukicha, Afrika ndiyo inaongoza. Mtumishi mmoja wa Mungu nchini Ghana amenaswa hivi karibuni akimwogesha mke wa mtu ambaye ni muumini wake kwa madai anamtakasa.
Picha ya mtumishi huyo ilipigwa kwa siri na kamera ndogo iliyotegwa eneo la tukio.
Habari zinasema mtumishi huyo (jina lake halikupatikana mara moja) alimwogesha mwanamke huyo wakati wa mfululizo wa maombi ya utakaso maarufu kwa jina la Deliverensi.
Baada ya kumaliza kumwogesha, alimfuta maji kwa taulo na baadaye kumpaka mafuta aliyodai yana upako wa ki-Mungu ‘Anointed’.
Ni vyema jamii ikaangalia upya sera za makanisa, hasa ya kiroho, wanayojiunga nayo kwani mengi hayafuati maagizo ya Mungu bali shetani.

No comments: