Mtu na wifi yake wanaswa wakijiuza
UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Firauni, sakata la mtu na wifi yake kunaswa wakifanya biashara ya ukahaba na kufikishwa mahakamani limewastajabisha wengi, Risasi Jumamosi linakutaka ukae mkao wa kula kupata kisa hiki.
Sakata zima liko hivi, Jennipher Anthony (21) Mkazi wa Tabata jijini Dar pamoja na wifi yake Mgeni Tumaini (35) Machi 13, mwaka huu saa 9 usiku walinaswa na polisi maeneo ya Buguruni Kwasokota jijini Dar wakiwa katika harakati za biashara yao ya ukahaba.
Mara baada ya kukamatwa na polisi, mtu na wifi mtu hao walipandishwa
kizimbani katika mahakama ya Hakimu Mkazi ya Sokoine Drive kwa kosa
hilo.
Wakizungumza na Risasi Jumamosi, ndugu wa watuhimiwa hao waliofika
mahakamani kwa ajili ya kusikiliza kesi hiyo, walimlaumu Mgeni kwa
kumpotosha wifi yake Jennipher na kumuingiza kwenye biashara hiyo haramu
wakati akijua kuwa ana umri mdogo.
“Jennipher ametoka Iringa kwa ajili ya kuja kutafuta maisha na
kufikia kwa wifi yake, kumbe walikuwa wakifanya biashara hiyo haramu
bila sisi kujua,” walisema ndugu hao kwa masikitiko.
Mbali na Jennipher na wifi yake, wanawake wengine waliopandishwa
kizimbani katika mahakama hiyo kwa kutokana na kise hiyo ni Asha Samson
(25) Mkazi wa Mburahati, Aisha Mohammed (35) Mkazi wa Kigogo pamoja na
Jenny Michael (19) Mkazi wa Mbagala na kusomewa shitaka la kufanya
biashara haramu ya ukahaba.
Akiwasomea mashitaka yao Kaimu Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama
hiyo Richard Magodi mbele ya Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo
Timothy Lyon alisema washitakiwa wote kwa pamoja walikana shitaka hilo.
Hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo aliihairisha kesi mpaka Machi
26 mwaka huu, huku watuhumiwa wakikosa dhamana baada ya kushindwa
kutimiza masharti na kupandishwa karandika kwenda katika Gereza la
Segerea mpaka kesi hiyo itakapotajwa tena.
No comments:
Post a Comment